Audio Mp3

audio song

Thursday, May 31, 2018

ALAMA ZA MWANAMKE ANAYEKUHITAJI KIMAPENZI 

May 31, 2018 12:40 PM

KARIBU kila kitu huwa na dalili zake. Mvua ina dalili, homa ina dalili, hata kwa mujibu wa mafundisho ya dini siku ya mwisho pia ina dalili zake. Kupitia hizo dalili, ndiyo hasa huwa tunajua uwepo au kutokuwapo kwa kitu.

Japo si mara zote mawingu yakitanda huwa mvua inanyesha, ila huwa mara nyingi yakitanda mvua hunyesha. Kilichokusudiwa hapa ni kwamba, kuna mienendo na mambo hutokea kutoa ufahamu wa kitu fulani.

Wanawake ni tofauti sana na wanaume. Matendo mengi yanayofanywa na wanaume ni wanawake wachache sana huweza kufanya, tena pengine hufanya chini ya viwango na mbinu husika zinazotumiwa na wanaume.

Yapo matendo mengi kama kukimbia, kupigana, hata jinsi wanavyowaza na kuamua. Ila hapa najadili kuhusu mapenzi.

Si mara zote mwanamke huwa anamwambia mwanamume hisia zake moja kwa moja, kama ambavyo wanaume wamekuwa wakifanya. Ndiyo kuna wanawake wana uwezo huo, ila ni wangapi? Ni wachache sana.

Katika jamii jukumu la kueleza hisia za mapenzi linaonekana hasa ni la kiume. Wanawake wamebaki kuwa wasikilizaji tu au kama akiwa naye kapenda kweli hubaki kuonesha hali hiyo kupitia ishara.

Wanawake wengi hufanya hivi badala ya kusema nini wanajihisi kwa kina fulani. Unamjua mwanamke anayekupenda wewe? Hata kama hajasema akiwa na ishara zifuatazao huyo atakuwa na hali ya hisia fulani za upendo na wewe.

(i)Atapenda kuongea na wewe, kila anapopata nafasi atapenda kuwa na wewe karibu mkiongea. Atakuwa makini na kufanya kila analoweza kuona kuwa anaheshimu mazungumzo yako na uwepo wako. Inaweza kuwa huwa anaongea na watu wengi, ila uongeaji wake utakuwa tofauti sana na akiwa na wewe. Kwako atakuwa na heshima zaidi na utulivu zaidi, tena akiwa ana ujasiri wakati mwingine atapenda kugusana na wewe muwapo katika mazungumzo yenu. Hata kama hakuna ulazima anaweza kugusisha bega lake kwako au hata kugongesha viganya. Yote anafanya katika hali ya kuipa furaha nafsi yake pamoja na kuonesha ni kwa namna gani kwako alivyo huru.

Mwanamke huwa muoga sana kugusana na mwanamume, ila woga huo hutoweka akiwa na hisia fulani nzuri juu yako. Hata kama ukimgusa bahati mbaya maeneo kama ya maziwa na hata kwenye makalio hawezi kukutukana wala kujisikia vibaya kama akifanyiwa na mtu asiye na hisia naye.

(ii)  Atakuwa na nidhamu kwako, ndiyo, anaweza kuwa mtu wa nidhamu siku zote. Ila hapa kwako itakuwa zaidi.

kwa kipindi chote anachokutana na wewe atahakikisha anaonesha hali ya nidhamu kwako na unyenyekevu. Kwake hali hii itakuwa na tafsiri mbili; kwanza anataka kuonesha kwamba wewe ni mtu muhimu sana kwake ila pili atataka uone raha na furaha kuongea na yeye.

Wakati mwingine nidhamu yake huwa kama pia imechangiwa na aina fulani ya woga, ila hufanya hivi katika namna ile ile ya kukuonesha ubora na hadhi katika moyo wako.

(iii) Atafanya kitu kwa ajili yako, hata mkiwa mmekutana pamoja halafu wewe ukaonesha una shida na kitu fulani, aidha nguo au hata kitabu, yeye kama pesa anayo atataka kukununulia.

Jambo hili kwake huwa ni katika hali ya kuweka alama katika maisha yako na kuonesha ni kwa kiasi gani ulivyo na umuhimu katika maisha yake. Hata nauli mkiwa pamoja atataka kukulipia ikiwa tu ana pesa za kutosha.

Atajitahidi kwa kila hali kukuonesha yuko tayari kwa ajili ya kukupa furaha na kuonesha umuhimu wako katika maisha yake.

(iv)  Kukupa zawadi, haijalishi ni ya gharama kiasi gani, ila atataka kukupa zawadi ikipatikana nafasi ya kufanya hivyo.

Zawadi ni kipimo cha thamani na kumkumbuka mtu. Yeye atafanya hivi katika hali hiyo na ili umfikirie zaidi. Tena akiwa mjanja zaidi anaweza kukupa zawadi zenye uashiriao wa mapenzi na kumbukumbu.

Kwa mfano anaweza kukununulia saa au kitu chenye maandishi yenye kujenga hali ya mapenzi na kuonesha dhamira yake kwako. Hapa wengi huwa ni waoga kutoa zawadi za maua au kadi, japo kuna wengine wana uwezo wa kufanya hivyo.

Woga wao unakuja kutokana na zawadi husika kuwa wazi sana kuonesha dhamira zao.

(v)  Kutaka kujua mengi kuhusiana na familia yako, ili kuonesha ni kwa namna gani anahitaji nafasi katika maisha yako, atataka kujua mambo unayoyapenda na kujua vitu muhimu katika familia yako.

Atataka kujua wewe ni wa ngapi kuzaliwa, kabila lako na asili yako kwa ujumla. Pia atataka kujua chakula na mavazi unayopenda, aina ya familia na mwanamke unayetaka kuwa naye katika maisha yako.

Kwa mwanamke mjanja yeye atakubana sana katika maswali ya namna hii, ila nawe ukitaka kumpa maswali atakujibu kwa namna ya majibu yako kwake yalivyo.

Kwa mfano; unaweza kusema unapenda mwanamke wa aina Fulani, ila kama yeye tayari kakuuuliza na umemjibu swali la mwanamke unayempenda atakujibu kwa mujibu wa jibu  lako. Hata kama ataongeza kitu ila si katika namna ya kutoa maana halisi ya kitu ulichoongea.

(vi)  Atata kuishi kwa namna unavyopenda, baada ya kujua wewe ni mtu wa aina gani kupitia maswali na mfumo mzima wa maisha yako, atataka kuishi namna unavyopenda ili uweze kuvutiwa naye. Kama atajua hupendi mwanamke mapepe hata siku moja hawezi kujichetua kwa kuamini kwa kufanya hivyo atakuwa anakufukuza.

Akijua hupendi mwanamke mwenye marafiki wengi wa kiume hata kama alikuwa nao atafanya kila njia kuachana nao. Yote atayafanya katika hali na namna ya kukuonesha kuwa yeye ni mtu anayekufaa katika maisha yako.

(vii)   Atakuwa na huruma zaidi kwako, akihisi una matatizo au unapitia katika hali ngumu ya kimawazo atataka kuwa karibu zaidi na wewe pamoja na kukupa maneno ya kukutia nguvu na imani zaidi. Hata siku moja hawezi kukuacha ukiwa unataabika kifikra na kuumia peke yako, katika kila namna atakayoweza atataka kuonesha ni kwa kiwango gani anaweza kukufuta machozi na kujenga tena tabasamu katika sura yako.

(viii)  Atazungumzia mipango yake ya mbele kwako, ili kukuvuta zaidi kwake ataweza kukueleza nini mipango yake ya baadaye na namna gani alivyo na dhamira ya kweli katika kufikia ndoto zake.

Atafanya hivyo kukufanya ujue yeye ni mtu mwafaka na bora sana katika maisha yako. Atataka ujue unapoingia naye katika uhusiano basi, utakuwa na mtu mwafaka katika maisha yako ambaye atakufanya uyaone maisha mepesi kwa usaidizi wake.

(ix)  Atakusikiliza kwa makini na kutekeleza unayopenda, kwa ajili ya kukuvuta kwake atakuwa makini katika kukusikiliza na kufanya yale unayopenda kufanyiwa au unayotamani kufanyiwa.

Hata bila kumtaka afanye yeye atafanya kwa umakini huku akiwa makini kuona mwitikio wako katika suala husika, akiona umefurahia atafanya hivyo kadri atakavyopata wasaa wa kufanya.

UKAWA wapigwa chenga

BUNGE jana 'liliupiga chenga ya mwili' Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) baada ya kupitisha makadirio ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.....

.....kwa mwaka ujao wa fedha bila uwapo wa mbunge hata mmoja wa upande huo, ikiwamo chama kikuu cha upinzani nchini Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Katika kikao cha jana cha Bunge kilichofanyika kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa saba mchana, hapakuwa na mbunge hata mmoja wa Chadema bungeni kutokana na kile kilichoelezwa na uongozi wa chama hicho kuwa wabunge wake wengi walikuwa mkoani Kigoma kushiriki mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Buyungu, Kuasuku Bilago.

Mwili wa mbunge huyo aliyefariki dunia Jumamosi kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) uliagwa juzi na wabunge jijini Dodoma kabla ya kusafirishwa kwenda Kigoma kwa ajili ya mazishi.

Huku ratiba ya vikao vya Bunge la Bajeti ikionyesha makadirio ya bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi yalipaswa kujadiliwa kwa siku tatu, Bunge jana lilitumia muda wa takribani saa nne kuyajadili na kuyapitisha huku viti vinavyokaliwa na wabunge wa Chadema vikiwa tupu.

Ratiba ya vikao vya Bunge la Bajeti inaonyesha kuwa makadirio ya bajeti ya wizara hiyo yalipaswa kujadiliwa bungeni kwa siku tatu kuanzia Jumatatu, lakini hayakuwasilishwa bungeni siku hiyo kutokana na Naibu Spika Dk. Tulia Ackson kutangaza kuahirisha shughuli za Bunge kufuatia kifo cha Bilago.

Juzi, Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi, aliwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara yake lakini hayakujadiliwa na Bunge kwa kuwa kulikuwa na shughuli ya kuaga mwili wa Bilango kwenye Viwanja vya Bunge.

Wakati wa kuipitisha bajeti hiyo jana, hakuna mbunge hata mmoja wa vyama vilivyokuwa na wabunge bungeni jana aliyewasilisha hoja ya kuzuia mshahara wa waziri, hivyo bajeti hiyo ya Sh. bilioni 65 kupita bila kupingwa.

Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu, aliyekuwa anaongoza kikao hicho, alisema kukosekana kwa mbunge wa kuipinga bajeti hiyo ni matokeo ya uchapakazi wa Waziri Lukuvi na wasaidizi wake.

Bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka huu wa fedha (2017/18) pia ilipita bila kupingwa na mbunge yeyote wakati wa Bunge la Bajeti la mwaka jana huku Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, akiwataka mawaziri wengine kuiga utendaji wa Lukuvi.

'TUPO KIGOMA'

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika, alipotafutwa kuzungumzia kutokuwapo kwa wabunge wote wa chama chake bungeni jana alisema: "Kimsingi wabunge wengi tupo huku Kigoma na wachache wana udhuru."

Mbunge wa Kibamba huyo alibainisha kuwa wabunge wa chama chake watarejea bungeni kushiriki vikao vya Bunge baada ya mazishi.

Wednesday, February 21, 2018

Walimu wa sekondari kufundisha Shule za msingi Serikali yatoa tamko

Serikali imesema mwalimu wa sekondari kufundisha shule ya msingi si kushushwa cheo na wala si jambo la ajabu.

Taarifa ya mkuu wa kitengo cha mawasiliano Ofisi ya Rais (Utumishi), Florence Lawrence imesema Serikali kuwapangia baadhi ya walimu wa sekondari kufundisha shule za msingi ni moja ya hatua za kuongeza ufanisi na kuleta mgawanyo sawa wa walimu katika shule hizo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro amekaririwa katika taarifa hiyo iliyotolewa leo Februari 20,2018 akisema hatua hiyo haimaanishi kuwa walimu wanaotoka katika shule ya sekondari kwenda kufundisha msingi wameshushwa cheo.

Dk Ndumbaro ametoa ufafanuzi huo katika kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako.

Amesema lengo la Serikali ni kuondoa upungufu wa walimu katika shule za msingi na kuimarisha utoaji wa elimu.

Katibu mkuu ameainisha kuwa sifa za kufundisha na kiwango cha elimu zinaendana na mabadiliko yanayotokea duniani, hivyo mwalimu mwenye elimu ya kiwango cha Shahada ya kwanza kufundisha shule ya msingi isionekane ni jambo la ajabu.

Dk Ndumbaro amewaambia watumishi wa umma kuwa, maendeleo katika sekta yoyote, ikiwamo ya elimu yanakuja na mabadiliko hivyo wayapokee na kufanya kazi ili kufikia lengo.

Monday, February 12, 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya February 13


Aslay, Nandy kuburuzwa mahakamani

Wimbo  wa 'Subalkheri Mpenzi', ulioimbwa na wasanii wa kizazi kipya Aslay Ishack na Nandy, umezidi kuzua utata baada ya mmiliki wa wimbo huo, Kikundi cha Tarab Asilia visiwani Zanzibar (Culture Music Club), .........Kudai kuwa watawaburuza mahakamani kwa kuwa Sh. 800,000 zilizotolewa kama fidia hawazitambui.

Katibu Mtendaji wa kikundi hicho, Taimur Rukuni Twaha, jana alisema wasanii hao kabla ya kuimba tena upya wimbo huo walipaswa kuonana na uongozi huo ili kukubaliana jambo ambalo hawakufanya hivyo.

Kwa mujibu wa katibu huyo, wasanii wa kikundi hicho waliopewa mgawo huo wa fedha ni waimbaji wawili (majina tunayo) ambao mmoja alipewa Sh. 500,000 na mwingine Sh. 300,000.

“Walichokifanya Aslay na Nandy kwenda kwa waimbaji wetu na kuwapa kiwango hicho cha fedha kwetu tunaona hakikubaliki na wametoa kama zawadi tu kwa sababu thamani ya wimbo wetu haulingani na kiwango hicho,” alisema Twaha.

Alisema kwa mujibu wa katiba ya kikundi hicho, ibara ya sita inaeleza nyimbo zote zilizoimbwa na kikundi ni mali ya kikundi na kwamba muimbaji, mtunzi na muweka sauti watakuwa na haki zao kupitia kikundi hicho.

Alisema kimsingi msimamo wao utabaki pale pale wa kuwafikisha mahakamani wasanii hao endapo watashindwa kutimiza masharti waliopewa na uongozi wa kikundi hicho.

Aidha, alisema masharti hayo hayatomhusu Aslay na Nandy peke yao bali na mwanamuziki Hussein Mmanga Faki (maarufu HamaQ) na mwenzake Mosi Suleiman kwa kuimba wimbo wa 'Mke wa Awali ni Wewe Aziza' ambao pia ni mali ya kikundi hicho.

“Tunafahamu kuwa nyimbo zetu wameziimba tena kwa lengo la kibiashara na wamekuwa wakipata fedha kupitia nyimbo hizo,”alisisitiza katibu huyo.

Alisema tayari wameshawaandaa mawakili wao, ambao wataisimamia kesi hiyo mahakamani iwapo wasanii hao watashindwa kutimiza masharti waliyopewa.

Akizungumzia suala hilo, Meneja wa Coconut FM, ambaye ni mwakilishi wa Aslay na Nandy, alisema kuwa wasanii hao watafikishwa katika uongozi wa Kikundi cha Taarab Asilia (Culture) ili kupata suluhu.

Alisema wao hawana makosa kutumia wimbo huo, kwani kabla ya kurudia kuuimba walishakutana na mtunzi wa wimbo huo Bakari Abeid ambaye sasa ni marehemu na kumalizana naye wakati wa uhai wake.

RC Mnyeti: Siwezi kutoa msaada kwa diwani wa CHADEMA , Labda Ahamie CCM Ndo Ntamsikiliza

Mkuu wa Mkoa wa Manyara,  Alexander Mnyeti amewataka madiwani wa vyama vya upinzani kujiunga na CCM ili waweze kushirikiana naye kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama tawala.

Amesema yupo tayari kupokea simu ya diwani wa CCM hata akipigiwa usiku wa manane, ili kumpa msaada lakini si diwani kutoka vyama  vya upinzani.

Akizungumza jana Februari 11, 2018 katika mkutano wa hadhara kata ya Haydom wilayani Mbulu, Mnyeti amesema ni vyema madiwani wa Chadema wakajiunga na CCM.

Amesema diwani wa Chadema ni ngumu kufanikisha maendeleo ya wananchi kwa madai kuwa, hakuna ambaye atamsikiliza akiwasilisha hoja zake katika vikao vya halmashauri husika.

"Hata hapa Haydom najua ni ngome ya Chadema hata mwenyekiti wa kijiji namuona ana damu ya CCM, sasa ondokeni huko mje huku tutekeleze ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 hadi 2020 kwa kuleta maendeleo," amesema Mnyeti.

Awali, mkazi wa kata ya Hayderer,  John Tluway aliuliza swali kwa mkuu huyo wa mkoa akitaka kujua sababu za mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Chelestino Mofuga kutofika kwenye kata hiyo inayoongozwa na Chadema.

Akijibu swali hilo, Mnyeti amempongeza Mofuga kwa kutokufika kwenye kata hiyo inayoongozwa na Chadema kwa maelezo kuwa diwani wa kata hiyo anapaswa kujiunga na CCM ili kufanikisha maendeleo.

"Mkuu wa wilaya ninakupongeza kwa wewe kutofika kwenye kata hiyo kwani ningepata taarifa umefika mara ya kwanza, mara ya pili na mara ya tatu ningekuwa na mashaka na wewe lakini hongera sana kwa kutokwenda,"amesema Mnyeti.

Pia, amewataka watumishi wa halmashauri hiyo kutekeleza na kufanikisha kwa vitendo ilani ya CCM hata kama hawana kadi ya chama hicho kwani ndicho ambacho kipo madarakani.

"Mtekeleze hayo kwa nia safi, hiyo ni sawa na imani kwani hata kanisani huwezi kusikia padri akimsifu Muhammad na pia kule msikitini imamu huwa hamsifu Yesu," amesema Mnyeti.

Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Mbulu, Nasaeli Sulle alimhakikishia Mnyeti kuwa wananchi wa Haydom wamejitambua kuwa walifanya makosa na kuchagua Chadema ila sasa wapo tayari kuwachagua viongozi wanaotokana na CCM.

Tanga RAHA- Sehemu ya Pili ( 2 )

 

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  

Rahma alizungumza huku akiwa ameishika bastola yangu huku akijipiga piga nayo mashavuni mwake, nakujikuta nikitoa toa miguno

Akautoa ulimi wake na kuanza kuuchezesha juu ya kichwa cha bastola yangu ambayo ina tundu dogo la kutolea risasi zisizo na idadi kamili.Jinsi ulimi wa Rahma unavyo zunguka juu ya kichwa cha bastola yangu kwa ndivyo nilivyo hisi risasi zikitaka kutoka, na kujikuta nikianza kukoroma kama mtu aliye banwa na haja kubwa kwenye choo cha foleni kubwa

ENDELEA

Rahma akazidisha kasi na kunifanya nitoe miguno mizito ya kimapenzi.Gafla raha zikakata, mithili ya umeme wa tanesco unavyo katika. hii ni kutokana na simu ya Rahma kuita kwa mlio mkubwa kiasi, Akanyanyuka na kwenda kuipoke

"Hallow mama"

"Nipo kwa rafiki yangu sinto chelewa kurudi"

Rahma akaendelea kuzungumza kwa lugha ya kiarabu, ambayo sikuielewa hata neno moja analo lizungumza.Akakata simu na kurudi nilipo

"Mama naye"

Rahma alizungumza huku akiwa amenuna

"Ana semaje?"

"Anataka nirudi nyumbani sasa hivi?"

Sikuwa na jibu la kuzungumza zaidi ya kumtazama Rahma na kuendelea kulidhaminisha umbo lake, lilivyo zuri na la kuvutia.Rahma akaishika bastola yangu kisha na kuitumbukiza mdomoni na mara hii akazidisha kuinyonya kwa kasi

Akasimama na kunikalia mapajani huku akiishika bastola yangu na kuiingiza kwenye ikulu yake ambayo ina joto kali.Rahma kama mwanamke aliye pagawa akaendelea kuikalia kwa nguvu huku akiwa anakizungusha kiuno chake, na kunifanya na mimi kutoa vilio vya mfululizo

Bastola yangu ikiwa ndani ya ikulu nikahisi inagusa sehemu ngumu ngumu, ambayo kila inapogusa Rahma akawa anakunja uso kama mtu anayepata maumivu

Rahma akaning'ang'ania shingoni kwa mikono yake huku midomo yetu ikiwa na kazi ya kunyonyana midomo yangu, mipana fulani huku kiuno cha Rahma kikiwa kinazidi kuzunguka

Rahma akajitoa kwenye mapaja yangu akasimama na kunivuta kwenye kochi nami nikawa nimesimama huku nikisubiri maelekezo yake

Sunday, February 11, 2018

Serikali yawasha moto Bungeni kuhusu madanguro, biashara ya ngono

Serikali imesema ina andaa mikakati itakayowezesha kudhibiti biashara ya ngono na uwepo madanguro nchini, hasa kwenye maeneo ya mijini.

Hayo yamesemwa jana Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe, Khalifa Mohammed Issa aliyehoji juu mpango serikali katika kudhibiti biashara ya ngono na madanguro ili kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU) nchini.

Akijibu swali la Issa, Dkt. Ndugulile alisema Serikali inaandaa mikakati mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kuhusu madhara ya biashara ya ngono kwa jamii pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wanaojihusisha na baishara hiyo, pamoja na kudhibiti uwepo wa madanguro.

Katika hatua nyingine, Dkt. Ndugulile alisema serikali inaendelea kuchukua hatua katika kudhibiti mila na desturi potofu zinazochangia maambukizi mapya ya VVU, ikiwemo ukeketaji na urithishaji wa wajane kwa ndugu wa mume, kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya mila potofu pamoja na kutoa hamasa kwa wakunga wa jadi wanaojihusisha na ukeketaji.

TANGA RAHA- Sehemu ya Kwanza (1)


MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

Ni siku ya utambulisho mbele ya wanafunzi wa shule ya sekondari moja jijini Tanga nikiwa mimi na mwalimu mwenzangu ambaye wa kike ambaye ndio tumetoka chuo cha ualimu na kupangiwa shuleni hapa

Akaanza mwenzangu kujitambulisha ambaye, akapigiwa makofi na wanafunzi kisha nikafwatia mimi kujitambulisha

"Mimi ninaaitwa Sir Eddy nitafundisha Biology na Chemisty"

Wanafunzi wote wakapiga makofi ma vigelegele hukt wakionekana kupendezwa na utambulisho wangu mfupi na wakueleweka.Muda wa masomo nikakabithiwa kuanza na kidato cha nne katika somo la Biology ambao ndio nao wanaanza mwezi wa kwanza wa muhula wa masomo.Nikaanza kuuliza mwanafunzi mmoja mmoja jina lake ili kuniwia rahisi kuwafundisha na kuwazoea kwa haraka

Nikaanza kipindi huku nikiwauliza uliza maswali ya mada walizo zisoma wakiwa kidato cha tabu, ili niweze kwenda nao sawia kwenye kufundishana

"Ulisema unaitwa nani, binti?"

"Rahma"

"Ehee elezea Reproduction(uzalishaji) kwa mwanadamu inakuwa vipi?"

Akanza kuelezea hatua moja baada ya nyingine kuanzia mtoto anavyo tafutwa hadi kuzaliwa bila hata kukosea.Wanafunzi wenzake wakampigia makofi huku wengine wakitaka kutokana na baadhi ya vitu alivyokuwa akivizungumza

Wakanipa ushirikiano mzuri hadi nikamaliza kipindi na kurudi zangu, ofisini nikisubiri kwenda darasa jengine

Muda wa kutoka ukawadia nikabeba begi langu lenye laptop yangu niliyo hifadhi vitu vyangu mbalimbali

"Sir ninaweza kukusaidia kubeba begi?"

"Rahma ndio unaweza kunisaidia"

Rahma yupo na mwenzake ambaye sikumuona darasani wakati nilipokuwa ninafundisha somo langu

"Unakalia wapi?"

"Maeneo sijui wanapaita Chuda, kitu kama hicho"

"Sir Eddy kwani Tanga wewe ni mgeni?"

"Nimgeni nina kama siku ya nne leo, tangu nije bado majina yana nisumbua sumbua kuyashika"

"Umetokea wapi?"

"Arusha"

Tukatembea njia nzima huku tukizungumza mambo mengi, kuhusiana na mji huu ambao nyumba zake zimepangika vizuri kwa mpangilio wa mistari mistari, nitofauti sana na mji kama Dar es Salaam.Tukafika nyumbani kwangu na nikawakaribisha na sote tukaingia ndani kuingia ndani

"Ehe sir Eddy umejitahidi?"

Rahma ni muongeaji sana kiasi kwamba hakuwa anampa mwenzake nafasi, ya kuzungumza na mimi japo hata kuchangia mada ya jambo tunalo lizungumzia

"Nimejitahidi vipi?"

"Chumba chako ni kizuri"

"Asante"

"Sir acha sisi twende tutakuja kukutembelea jumamosi"

"Sawa karibuni"

Wakaondoka na kuniacha nikiendele na shughuli zangu za kawaida, ikiwemo kupika chakula cha mchana, nilicho kijumlisha na chakula cha usiku.Nikaendelea kufanya kazi kwa juhudi siku zote za kazi yangu, huku upendo wangu wa kuipenda kazi yangu ukizidi kuongezeka kadri ya siku zilivyozidi kukatika

Thursday, February 8, 2018

Hoteli ya Hyatt Regency Yatangaza Chumba cha Milioni 22..4 kwa Usiku mmoja tu wa Valentine Day...Kazi Kwako Mdau siku hiyo ya WAPENDANAO

Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam juzi ilitangaza ofa ya chumba cha Sh22.4 milioni katika Usiku wa Valentine na kusema kuwa Watanzania mbalimbali wamekuwa wakipiga simu kutaka kujua kama ni bei halisi na wengine kuomba punguzo.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo, Denis Glibic alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu chumba hicho na namna watu walivyolipokea tangazo hilo.

Glibic alisema tangu watangaze ofa hiyo ambayo ni kwa ajili ya wapendano katika sikukuu ya Valentine, wamepokea simu nyingi kutoka kwa Watanzania wakitaka kujua kama kweli hilo ni tangazo lao halisi na wengine wakitaka wapate nafasi hiyo kwa punguzo la bei. 

Kuhusu chumba hicho ambacho kinatumiwa na marais mbalimbali duniani wanapokuja nchini, meneja mwendeshaji wa hoteli hiyo, Timothy Mlay alisema, kwa kawaida bei yake huwa ni Sh11.4 milioni kwa siku.

Alisema pamoja na kuwapo kwa malalamiko ya maisha magumu, wanaamini watu watapatikana kwani kwao kuanzia Desemba mpaka sasa ni kipindi ambacho hupata wateja wengi.

Alisema huduma zitakazotolewa kwa wateja wa chumba hicho siku hiyo zitakuwa tofauti kwa wateja wengine, kwani mbali ya kwenda kuchukuliwa na gari la kifahari eneo wanaloishi, pia watapatiwa zawadi za mapambo ya mwilini yenye madini ya Tanzanite